Friday, March 27, 2015
2:28 PM
| Posted by
Unknown
|

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
Siku moja baada ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kusitisha makundi yanayokwenda kumshawishi kugombea urais, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, amempongeza kwa kutii agizo la chama hicho.
Nape amesema hatua hiyo ya Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli ni nzuri kwa kuamua kusitisha makundi kwenda kumshawishi agombee urais, ambayo kwa siku chache mfululizo yalikwenda
nyumbani kwake Monduli na mjini Dodoma kwa nia hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana akiwa katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulahman Kinana wilayani Same, Kilimanjaro, Nape alisema anampongeza Lowassa kwa kuwa amekubali kuheshimu kanuni, taratibu na Katiba ya chama ambayo ndiyo inatakiwa kufuatwa na kila mwanachama wa CCM.
Jumanne wiki hii, Nape alimuonya Lowassa kujiepusha na makundi hayo kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka kanuni na taratibu za chama na kwamba, hali hiyo inamkosesha sifa ya kuteuliwa kugombea urais kupitia CCM.
Nape alisema walimtaka Lowassa, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM azuie makundi yanayokwenda nyumbani kwake kwa ajili ya kumtaka agombee urais kwani kilichokuwa kinafanyika ni kuanza kampeni kabla ya wakati.
“Kilichokuwa kinafanyika ni kuanza kampeni kabla ya wakati na kwa mujibu wa chama chetu ni makosa, maana anakiuka taratibu na kanuni za chama. Hatuwezi kukaa kimya wakati kanuni zinavunjwa wazi, hivyo nimpongeze Lowassa kwa kutii agizo la chama,” alisema Nape.
Kuhusu shutuma kuwa kauli anazozitoa siyo za chama bali zake binafsi, Nape alisema yeye ndiye msemaji pekee wa chama na hakuna msemaji mwingine, hivyo kauli zinazotolewa ni za chama na siyo zake.
“Kanuni na taratibu ambazo nazisimamia zipo miaka mingi kabla ya mimi kuzaliwa. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM nchi nzima niko peke yangu, hivyo lazima nisimamie misingi ya itikadi pamoja na kanuni na katiba ya chama chetu. Kwa nafasi yangu siwezi kukaa kimya wakati kuna watu wanakosea,” alisema Nape.
Akizungumzia kuhusu wapambe wa makada wanaotaka urais, Nape aliwataka kuwa makini wasije wakawaharibia sifa wagombea wao.
“Ni vizuri wataka urais wakawa makini na ushauri kutoka kwa wapambe wao kwani wanaweza kuwasababishia kukosa sifa ndani ya chama, nawashauri wote wanaotaka kugombea urais kupitia CCM kutowasikiliza wapambe wao kwa kila wanachoambiwa, maana kuna ushauri mwingine unaweza kuwakosesha sifa za kugombea urais,” alisema Nape.
Waziri mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli Edward Lowassa
Waziri mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli Edward Lowassa
Alisisitiza kwamba, kwenye hilo si kwa wapambe wa Lowassa tu, bali ni kwa wapambe wote waliopo nyuma ya makada wanaotaka kugombea urais mwaka huu.
“Ni muhimu kwa makada wote kuhakikisha wanaheshimu kanuni, taratibu na miiko ya chama ili wawe salama, kinyume cha hapo watajipoteza sifa,” alisisitiza Nape.
Aliwahakikishia makada wa CCM kwamba chama hicho kitatenda haki kwa kila anayeomba nafasi ya uongozi na hakuna atakayenyimwa haki yake.
“Kwa wote ambao watakuwa makini katika kuzingatia kanuni na taratibu za chama, haki zao zitalindwa, lakini wale ambao watakiuka kwa makusudi, hao hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao,” alisema na kuongeza:
“Ndio maana tunaendelea kuwakumbusha makada wote wazingatie kanuni na katiba ya chama chetu. Kinyume cha hapo watakuwa wanajinyima wenyewe haki ya kuomba ridhaa ya kugombea kupitia chama hiki.”
Juzi Lowassa aliwataka wanaotaka kumshawishi wasubiri utaratibu utakaotolewa na chama hicho kuhusiana na suala hilo.
Alitoa kauli hiyo baada ya kutembelewa na vijana 60 waendesha bodaboda kutoka wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya.
Chanzo: NIPASHE
Subscribe to:
Post Comments
(Atom)
TOKOMEZA MAUAJI YA ALBINO

Find us on Facebook
Popular Posts
My Blog List
-
Startimes Kuonyesha Safari Nzima ya Warembo wa Miss Universe Tanzania - Na Mwandishi Wetu VIPINDI vya mashindano ya Miss Universe Tanzania 2025 vinatarajia kuanza kuonekana kuanzia leo Julai 25 mwaka huu katika king’amuzi cha S...3 minutes ago
-
WAJUMBE WA KAMATI JUMUISHI YA UENDESHAJI PROGRAMU YA MIFUMO HIMILIVU YA CHAKULA 'TFSRP' WAKUTANA PEMBA - Wajumbe wa Kamati Jumuishi ya Uendeshaji wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula (TFSRP) wamekutana katika Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba, k...1 hour ago
-
BI. SAKINA MWINYIMKUU: JENGENI UTAMADUNI WA UTENDAJI UNAOTEGEMEA MATOKEO - Dodoma, Julai 25, 2025 Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bi. Sakina Mwinyimkuu, amew...1 hour ago
-
Teknolojia : JAB Yakabidhi Press Card kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Michuzi Media Group - ●Waandishi Wengine Watakiwa Kuhakiki Viambatisho Katika Mfumo Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandis...1 day ago
-
RC Kihongosi Asikiliza na Kutatua Kero za Wamiliki na Wafanyakazi wa Saluni, Jijini Arusha. - [image: WhatsApp%20Image%202025-07-23%20at%2007.58.16] [image: WhatsApp%20Image%202025-07-23%20at%2007.58.14] [image: WhatsApp%20Image%202025-07-23%20at%20...2 days ago
-
Why are Japanese Cars so popular in the Arab World - Japanese cars have firmly established their presence in Arab markets, becoming a symbol of quality and reliability. The continued demand for these vehicl...1 week ago
-
สมัคร wing888 VIP เว็บตรงคุณภาพสูง และบริการคุณภาพ - Wing888 vip เป็นหนึ่งในชื่อที่น่าสนใจโดยเฉพาะสำหรับผู้ที่ให้ความสำคัญกับความปลอดภัย เสถียรภาพ และระบบการให้บริการที่จริงจัง ความเป็นส่วนตัวและความซื่อสัตย...2 months ago
-
BENKI YA STANBIC YAFIKIA TAMATI KAMPENI YA TAP KIBINGWA KWA SHANGWE - • TZS milioni 7.5 zimetolewa kama zawadi kwa wateja 15 waliotumia Visa Debit Card zao kwa miezi mitatu • Washindi wengine watano wajishindia TZS 500...3 months ago
-
KIWANJA CHA NDEGE SUMBAWANGA CHAFIKIA ASILIMIA SITINI YA UJENZI. - Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga umefikia asilimia sitini ya utekelezaji wake. Taarifa hiyo imetolewa mbele waandishi wa habari leo Machi 26, 20...3 months ago
-
Majina ya Blog Zinazoanzia na Herufi ya V - *1. VOA Sauti ya America * www.voaswahili.com *2. Vijimambo* lukemusicfactory.blogspot.com4 months ago
-
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025 - Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini ke...4 months ago
-
ZANZIBAR: UBALOZI WA NORWAY TANZANIA WAIPONGEZA TAMWA-ZNZ UTEKELEZAJI MRADI WA SWIL. - *Maafisa Ubalozi wa Norway wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa TAMWA-ZNZ mara baada ya kumaliza mazungumzo katika ofisi zilizopo Tu...3 years ago
-
AUDIO | Harmonize - Kushoto Kulia | Download - *DOWNLOAD* Listen to Harmonize - Kushoto Kulia byDJ Mwanga on hearthis.at5 years ago
-
-
Ufafanuzi wa TCRA kuhusu kuondoa chaneli za runinga zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka ving'amuzi vya Azam, Multichoice na Zuku - Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imefafanua kuhusu kuondoa Channel za Televisheni za ndani zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka Ving’amuzi vya Azam, Multic...6 years ago
-
MSANII ROSE MUHANDO: SIOGOPI WANAONISEMA VIBAYA - Rose Muhando. STAA wa nyimbo za Injili, Rose Muhando amefunguka kuwa, haogopi watu wanaomsema kwa ubaya kila kona bali anaangalia kile kilichomsababisha ku...8 years ago
-
VIDEO: SNURA AONGELEA KUFANYA KAZI NA DON JAZZY..! - Kila mtu alilipokea kwa style yake hili suala la mtayarishaji na msanii mkubwa wa muziki barani Afrika *Don Jazzy *kujirecord video akiimba wimbo wa Chura ...8 years ago
-
PIKIPIKI YAZUA HOFU BAADA YA KUTELEKEZWA MWAKA MZIMA JIJINI DAR ES SALAAM, UKIIKARIBIA, IKIIGUSA INAJIWASHA POLISI WAGWAYA KUIPELEKA KITUONI - Mwananchi akipita kwa kuikwepa pikipiki yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika Kituo cha waendesha...8 years ago
-
-
MATUKIO MBALI MBALI YA ZIARA YA KAMPENI ZA MGOMBEA URAIS WA UKAWA KUPITIA CHADEMA KATIKA JIMBO LA HAI, MKOANI KILIMANJARO - *Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipokelewa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Hai ...9 years ago
-
Bunge Lamkingia Kifua Zitto Kabwe......Lasema Bado ni Mbunge Halali na Spika wa Bunge ana Mamlaka Kisheria Ya Kutengua Maamuzi ya CHADEMA - Ofisi ya Bunge imesema haijapata barua yoyote kuhusu kuvuliwa uanachama kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema). Kauli ya hiyo ya Bunge im...10 years ago
-
MAPACHA 6 WALIOZALIWA MWAKA 1983 NCHINI UINGEREZA SASA NI WAKUBWA NA WAMENZA KUWA NA FAMILIA ZAO - * Bwana Na Bibi Grahan Walton wakiwa na mabinti wao sita pamoja na mjukuu wao* * Mapacha hao wa kike wakati wana miaka mitano (Kushoto kwenda kilia) Luci...10 years ago
-
New Song WAKAZI-BIGGIE - Download Here - *Wimbo mpya kutoka kwa Wakazi - Biggie* www.aloyson.com10 years ago
-
-
-
-
-
-
-
-
0 comments:
Post a Comment